Psalms 19:1-4

Utukufu Wa Mungu Katika Uumbaji

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 aMbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 bSiku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.
4 cSauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.

Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Copyright information for SwhNEN